NIONAVYO MIMI: Harry Kane muda wako wa kubadili mabao kuwa mataji. - ⚽Jumba La Michezo⚽

House of History, Sports & Movies

Breaking

Thursday, April 4, 2019

NIONAVYO MIMI: Harry Kane muda wako wa kubadili mabao kuwa mataji.

Tokeo la picha la harry kane


Na: bakari bakari jr
Simu: 0659767121

“I don’t see anyone endowed with talent affirming his desire to go to Spain. It’s a Championship its great disorder.” Arsenal Wenger on Henry

Baada ya Thierry Henry kucheza miaka nane ndani ya kikosi cha Arsenal kambi yao ipo kule Kaskazini mwa London huku akiwa ametwaa mataji yote ya pale Uingereza nikiwa na maana Premier League, FA Cup na Carling Cup kwa sasa Carabao, Henry ambaye kafunga mabao 175 kwenye EPL na mchezaji wa tano wenye mabao mengi. Henry amabye mwaka 1998 alitwaa kombe la dunia akiwa na kikosi cha Ufaransa na alitwaa euro cup 2000, kitu pekee alichokuwa kabakiza ni ilikuwa kutwaa taji la UEFA Champion League.

Wakati anahojiwa na waandishi Thierry Henry alikiri kuwa anataka kutimkia Hispania na lengo kubwa ni kutwaa taji la UEFA Champion League, Wenger hakuwa na chazaidi kinachoweza kumshawishi Henry kubaki Arsenal ndipo akasema kuwa “Sijawahi muona mtu yeyote ambaye amejaliwa na kipaji akijitangaza tamaa yake kwenda Hispania, Klabu bingwa ni ugonjwa wake” baada ya kusajiliwa 2007 na FC Barcelona mwaka 2009 alitwaa kombe la ndoto yake ya kuchukua taji ya UEFA Champion League ilitimia, wakati huo Barcelona wanabeba mataji matatu (Treble Won).


Picha inayohusiana

Harry Kane ambaye kwa sasa ni mfungaji wa mabao kwenye kikosi cha Tottenham Hotspur na timu ya taifa akiwa first choice striker, anafanya kazi ya kupachika mabao ya kila aina kila uchao. Akiwa na Tottenham Hotspur miaka kumi sasa amefunga zaidi ya mabao 164 kwenye Ligi mafanikio yake makubwa kwenye timu hiyo ni kuishia nafasi ya pili ya Kombe la Ligi mwaka 2015.
Harry Kane amekuwa akishinda Player of Month mara kadhaa na Player of year na hata kutwaa Golden boot katika FIFA World Cup 2018 kule nchini Russia. Lakini mpaka sasa ni miaka kumi yuko Spurs bila taji la aina yoyote huku Harry Kane anaenda kutimiza umri wa miaka 26 majira ya joto, ikiwa miaka mingi katumia kuichezea Spurs pasi na taji.

Harry Kane akiendelea kubaki Tottenham hatoshinda taji lolote kwa sababu ya kwanza Miujiza kwenye soka utokea mara chache na sababu ya pili Tottenham haina uwezo wa kuleta World class player kwa ajili ya Ushindani zaidi.

Picha inayohusiana

Miujiza ya Leicester City kutwaa EPL katika msimu wa 2015/16 kwa kweli ile ilikuwa miujiza ya kisoka huku timu yao ikiwa well organized and Committed baaada ya kushika usukani wa Ligi, Lakini pia walikuwa na bahati wachezaji wao katika msimu 2015/16 hawakupata majeraha jambo ambalo lilifanya klabu hiyo lichukue kombe la msimu huo. Lakini mchezaji kama Ng’olo Kante baada ya kuona hali ile haiwezi kujirudia basi akaachana na safari ya Leicester na kujiunga na Chelsea ambapo pia alitwaa taji la EPL. Swali la kawaida tu tangu Euro Cup 2004 Ugiriki waishangaze dunia nchi gani tena imefanya hivyo? Miujiza hii kwenye soka inatokea mara chache tena baada ya miaka mingi, ndio maana wakina Kante, Riyadh Mahrez baada ya kufanya miujiza hiyo mmoja akaenda Chelsea mwingine akatimkia Man City.

Kwa hali ya Tottenham haina uwezo wa kumleta mchezaji mwenye thamani ya zaidi euro million 60 kutokana na soko la usajili ulaya lilivyokuwa, kama timu inashindwa kuleta hawa World class Player majukumu ya timu anakuwa nayo Harry Kane ambapo akipatwa na jeraha basi fomu nzima ya timu inapotea na kuanza kupoteza michezo yao na ndio maana wachezaji kama Luka Modric aliondoka mapema baada ya kupata ulaji Real Madrid, lakini pia Gareth Bale alitambua hilo akaona ni vyema kurukia Meli ya Madrid for Career growth and development, Kyle Walker nae katimkia Manchester City tangu 2017, hawa wote wana mataji Modric na Bale wametwaa UEFA Champion League, La Liga, Club World Cup, Copa Del Rey. Kyler Walker ana taji la Premier League na Vikombe viwili vya Ligi.

Tokeo la picha la harry kane

Harry Kane uenda anatamani sana kuondoka timu yake hiyo ya utotoni Tottenham lakini anawafikiria maelfu ya mashabiki wa klabu hiyo ambayo ambao wote wanamuangalia yeye kwa furaha huku wakimuimbia nyimbo ya “he’s one of our own”, hali hii inakuwa kama legend wa Udinese Antonio Di Natale ambaye alikubali kubaki Udinese pasi na kushinda taji lolote. Di Natale akiwa na  25  kabla hajafika miaka 30 alishafunga mabao 47 kwenye Serie A katika misumu mitano kuanzia 2009 mpaka 2014 Di Natale alishafunga mabao 120 kwenye ligi akiwa na miaka kati ya umri wa miaka 31-36 akiwa mchezaji wa sita kwa mabao kwenye seria A. Lakini alikataa kuondoka mara zote huku akisisitiza kuwa anabaki Udinese. Au anataka kuwa kama Steve Gerald ambaye juu ya kutakiwa na klabu nyingi kubwa Ulaya alibaki Liverpool kuichezea kwa mapenzi yake yote huku akitwaa taji la Klabu bingwa Ulaya jambo ambalo Tottenham hawawezi kufanya japokuwa wako kwenye hatua ya robo fainali.

Kama Kane anataka kuendelea kusikiliza nyimbo “he’s one of our own” wakati akiwa katika uwanja wa White Hart Lane basi aendelee kubaki Spurs lakini kama anahitaji mataji basi akusanye virago vyake akaanze maisha mapya nje ya Spurs, kama walivyofanya wakina Henry, Van Persie, Mahrez, Bale, Modric, Walker wakati sasa wa kubadilisha mabao yake yazae mataji.

No comments:

Post a Comment

Pages